Jinsi ya kuishi kwenye frequency za uwezo wako wa ndani

 

Bonyeza picha kusikiliza sauti za Frequency

Mwili wako ni kama kioo cha frequency huakisi frequency inayo ingia , tendo linalo fanywa na mwili ni matokeo ya frequency iliyo ingia , mfano unaweza kumuona mtu mwenye chuki na kitu kwa vitendo vyake kulenga kitu au mtu huyo na hata maneno yake. Mwili huitikia na kutii frequency , mwili hupokea  frequency kutoka kwenye chanzo kikuu(akili ya hazina) na pia hutuma frequency Kwenda kwenye akili ya hazina kwa kupitia milango ya fahamu na hisia,mtazamo,tabia na chakras.

Chakras ni vituo 7 vya nishati kwenye mwili wa mwanadamu kila kituo kina rangi, sauti(note ya mziki) , hisia yake na somo lake la kiroho.

Hivyo unapobadili rangi unazojizungushia,sauti unazo sikiliza (mfano 528 Hz), Mawazo unayoamua kushilia, unapoamua fikra zako kuwa huru, yaani kupuuza  hoja za kisiasa, ki-mifumo ya elimu , ki dini,  ambazo hujengea watu hali ya kitu flani ni hivi na kufanya fikra zao zisifafanue jambo wakiamini tayari limesha fafanuliwa na ELIMU,DINI,SAYANSI AU SIASA.

Toa Fahamu yako kifungoni ipe uhuru wa kujipambanua iachilie yenyewe ina jua pa Kwenda inawajua watu wake, na watu wake wanaijua tangu siku unazaliwa. Mambo yatakwendea kwa namna ya ajabu sana,

Kuwa mtu asie na kiburi , kuwa mtu mwenye shukrani, ili usivamiwe na bila yeye mimi siwezi , bila yeye nisinge fika hapa, usimavamiwe na hapa nilipo siwezi kufika pale bila mtu flani kuninyenyua.

Wewe ni sawa na mbegu ya mmea ambayo inauwezo wa kuota hata pale jua likiiunguza sana lakini siku ikipata maji ikiwa kwenye udongo huota kwa furaha. Kumbuka mvua inanyesha bila kujua imefurahisha vitu vingapi, acha kuabudu msaada kuwa na shukrani peke yake ndio inatosha. Kama ambavyo mbegu haina mdomo haijaiambia mvua inyeshe lakini inanyesha kama utaratibu wake au jukumu lake.

Unatakiwa kutambua shali zikuzote hutaka malipo ila heri hakuna anayeweza kuilipa na haitaki malipo. Epuka kutoa huku unasema mimi ndio nimempa , au nimekupa kitu flani lakini unanitusi, hauniheshimu, umenikimbia, umenisaliti wote ni moyo wa giza. Toa kama desturi , Fanya unacho kiweza usifanye usichokiweza na wala usisicho kiweza kisikupe stress kwa maana ungekuwa unakiweza ungekuwa na uwezo nacho timiza majukumu unayo yaweza ili upate amani(high frequency).

Mwili hutenda kulingana na Frequency unayo ichagua wala hauelewi maneno wala lugha yoyote hutumikia frequency ulio ipokea ndio maana hata uchawi ni frequency ilitengenezwa kulenga mwili wako pindi unapo ungana nayo basi inaanza kukuathiri na mwili unatumikia frequency sio maneno, au lugha yoyote. Mtoto mwingine akikuta mama yake analia naye anaanza kulia , kwa kuwa yeye yupo kihisia zaidi kuliko mtu mzima, kwamba mwili wake unatumikia frequency iliyo zunguka hapo ya huzuni nayeye anajikuta analia.

Kabla hatuja endelea nitoe lai ninapo sema Malaika usifikilie picha ya kiumbe flani , ni dhana ya kumaanisha high frequency tabaka flani karibu na nguvu kuu tukufu takatifu ya juu kabisa.

Kwenye masomo tuliyo soma nyuma tulijifunza kwamba Malaika wakuu, Roho za Nuru, na Mababu Wema humtembelea mtu anapokuwa kwenye High Frequency, Pia tukasema Roho wasumbufu , mizigo ya mababu, na Nguvu za giza huja kwenye Low Frequency.

Namna ya haraka ya kujikinga athari ya Low Frequency ni pale unapo ziona hisia hizo za low frequency ziepuke kwa kuchagua upendo, Tafakari, Msamaha, Shukrani au nia njema kulingana na hisia iliyo kuja. Kwa maana hizi ni ngao zako za Frequency ya juu.

Ulimwengu wa roho unaingiliana na Mawazo yako hivyo kwa kubadilisha frequency, unabadilisha roho unazovutia.

Katika elimu za kiroho utakutana na kauli wewe sio huyo, au wewe sio masikini , au mwingine ataenda mbali atakwambia ramani yako ya maisha ilichorwa kabla hata hauja zaliwa na ukiipata ramani yako basi kwenye maisha haya utapata kufahamu ufanye kipi na kipi usifanye.

Elimu ya Unajimu wa Kale ndio iliyo leta Imani za Dini na Sayansi za kiwango chochote unacho ona leo, watu wakale waliangalia mzunguko wa sayari na magimba mengine angani na kuhusianisha na maisha ya viumbe duniani , walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kutabili matukio. Elimu hiyo ya kupata majibu kutokana na mzunguko wa sayari iliingia kwenye elimu ya unajimu.

Ebu tuangalia uhusiano wa unajimu au unajimu wako unamaanisha nini kwenye maisha yako ??

Unajimu utakupa au utakuonyesha Frequency yako ya Asili frequency uliyo zaliwa nayo, pia unakuonyesha uwezo wa juu (Uwezo wa Asili) , Karma ya zamani (Low Frequency)  na unajimu huo huo utakuonyesha eneo ambalo kwenye maisha unatakiwa kutoa mwanga , au huduma.

Zana ya kila mtu ana ubora wake na uzaifu wake inatoka hapa , ni kweli kila mtu alizaliwa na uwezo wake mkubwa wa pekee(High Frequency),  na alizaliwa na uzaifu pia(Low Frequency), na yote haya unayaona kwenye unajimu wa mtu.

Sasa ulivyo zaliwa kila sayari ilikuwa sehemu flani, kama vile tuseme ule muda ulizaliwa sayari ilikuwa inatembea lakini ilikuwa imefika mahali flani muda huo unazaliwa wewe , lakini kuzaliwa kwako bado yenyewe ina endelea na safari yake tu, sasa kulingana na imefika wapi kwenye safari yake nguvu yake huathiri maisha yako. Ndio maana utaona kuna nyakati nzuri unapitia na mbaya zinakuja pia, ukiwa na elimu unakuwa na msimu wa kukusanya na msimu wa kupoa kwa kuwa ukipisha na majira yako mwenyewe utakutana na hatari , hasara na mambo yaliyo faa, hivyo kumbuka unatakiwa kuchuma na kukaa kivulini kusubili msimu wako.

Msimu wakuchuma ukiwa haujui wala hauelewi ukapita hauja jipanga ndio utalaumu watu mpaka ukome.  Sasa safari ya sayari angani  hukukumbusha wewe somo, hukulazimisha kuponya,hukuvuta kwenye mwanga au giza.

Ni jukumu lako kujua ramani yako , na ufahamu wewe ndio dereva.

Jua lilikuwa wapi wakati unazaliwa , Hapo lilipo kuwa panahusiana na nini ?? basi wewe hapo ndio jukumu roho yako ilikuja duniani. Ukiishi jukumu hilo hakuna uchawi wa mtu wa kukuangusha wewe , Ukiishi jukumu hilo upo kwenye uwezo wako mkuu mababu wema , Malaika wema wanakuwa na wewe muda wote kukuunga mkono ili jukumu litimie hapa duniani , Kuishi jukumu lako ndio hapo husema nyota yako ina waka sana, hapo hatima yako inafunguka kabisa , unawaka kama taa kwenye giza nene.

Hivyo ulimwengu haukuamrishi bali unaitikia kama redio inavyopokea kituo unachochagua, ndivyo hivyo  maisha yako yanavyokujibu kulingana na ulivyo chagua.

Ukiwa kwenye low frequency unavuta mambo hasi mfano huzuni, watu wabaya, kukwama,magonjwa, na mambo mengine kama haya ya giza.

Ukiwa kwenye High Frequency , unavuta fursa,afya,wingi,mahusiano mazuri, mafanikio. Frequency yako ndio dua/sala yako halisi. Ulimwengu unasikia kile unachotuma, na si kile unachosema.

Kwa hiyo nini ufanye sasa.

Roho yako inajua cha kufanya sema umeifunga na mitazamo mingi ya kidini,kielimu,kifamilia,kimakundi,kisiasa,kijamii. Unatakiwa kuiacha huru ili iishi kusudi la yenyewe kuwepo hapa duniani, inajua wapi itapata ufahamu wa kutimiza kusudi lake , inajua watu walio zaliwa kwa ajili ya kukusaidia katika dunia ya nyama kutimiza kusudi na roho za mababu zako wema utake usitake wapo Pamoja na wewe ili kukuongoza maana ndio wasimamizi wa ukoo wako wewe.

Huwezi kuhusiana na ulimwengu wa kiroho kwa wema kama akili yako ipo na mawimbi ya beta(KIFUNGO cha mitazamo mingi ya kidini,kielimu,kifamilia,kimakundi,kisiasa,kijamii), Ufahamu wako mkuu , ubunifu na uwezo wa ndani yako unakuwa mubashara wakati akili ipo kwenye mawimbi ya ALPHA,THETA na DELTA (DELTA_ndio maana watu hulazwa ili mwili ujiponye).

Beta huzima yenyewe ukiwa umelala hata kama haujui, beta ikizima jicho la tatu linakuwa wazi kabisa bila wewe kujua, ukiwa haufahamu kutembea na fahamu Beta ikiwa imelala ndio una kuwa una ota mazingizonge , wachawi wanakuwangia watakavyo kwa kuwa malango ya kiroho yapo wazi.

Ni hatari kutokufahamu kitendo hiki cha kiroho, maana fahamu zako huelea kama hazina mwenyewe,

Zoezi la muhimu ili kuzinduka ni ku Jifunza namna ya Kuzima Beta, kwa utashi wako wewe ukijifunza namna ya kuzima mawimbi ya beta basi  ndio kujitambua kwenyewe.

Watu wanafundisha Meditation, wengine wanafundisha kufungua jicho la tatu, mimi nakuambia jifunze kuzima Beta , maana ikizima unakuwa kwenye Alpha na Theta , na ukiwa kwenye Alpha na Theta jicho la tatu linakuwa wazi bila kulazimisha.

Na vyote hivyo mazoezi ya meditation, elimu sijui ya kujitambua, sijui mazoezi ya jicho la tatu, sijui dawa ya kutoa uchawi, sijui kusafisha nyota, sijui kuombewa, sijui kuomba kwa yesu na mambo yoyote ya namna hiyo, vyote hivyo hulenga kuweka kwenye utulivu wa ALPHA na THETA ili roho yako ichukue utawala, iwe na nguvu yake , iwe na usawa wake wa asili.

Hata kupata Elimu huwa tuna elimisha BETA, ili kupata uthibiti wa mambo kadhaa, Beta ni mawimbi yanayo funga kabisa uelewa wa ndani ya mtu, beta ni mawimbi watu huwa wategemezi wa kifikra, beta inataka kujua kila kitu kwenye ulimwengu wan je, hivyo yule anaye jua vitu vingi vya nje huwa wengi wanamtegemea kwa maarifa. Mara zote BETA yako kila kitu isicho kijua, itakwambia hauwezi hiki, wakati ukiweza kuizima akili ya fahamu itakueleza kwa fahamu na uwezo wako halisi. Uwezo wa ndani ndio hiyo wengine wanaita kipaji au sijui genius yaani ule uwezo wa kufanya kitu kwa ubunifu bila kujifunza darasani.

Hizi Ni njia ninazo zipendekeza mimi kwa ajili ya kuthibiti SHETANI WA KWENYE VITABU VYA DINI (BETA).

1.Itoe akili yako kwenye mawimbi ya beta kwa kutumia sauti maalumu, sauti ya Nota za muziki, kila nota ina mlio wake. Ivi unajua kwanini muziki ni burudani ?? kwa nini mziki wengine unawatolea stress ?? ivi unajua mzuki wa mtu mwenye kipaji unadumu ?? haukinai kabisa kwa kuwa una mitetemo iliyo tiba, wenzetu wazungu wanafahamu hili tangu zamani, ndio maana sisi kwa ajili hautujui basi ndio sisi hujifunza kutoka huko.

Nilikwambia kuhusiana na chakras , chakra zikiwa kwenye usawa basi mwili na roho huungana na kufanya kwa usahihi wake .

Sasa unatakiwa kuipigia kelele BETA hadi izime , ufanya hivyo kwa kuliza sauti ya kila chakra kwa angalau dakika 3-5, mfululizo hadi chakra zote 7  kila chakra ina nota yake.

A.liza sauti ya chakra

B.fikiria rangi ya chakra

C.kuwa mvumilivu kwa dakika tatu. Huku sauti hiyo ikilia masikioni

Chakras frequency huwa na kipimo kwenye sauti (HZ)


Bonyeza picha kusikiliza sauti za Frequency

i.Mzizi (uti wa mgongo) rangi yake ni nyekundu note C(do), frequency 262 Hz, hisia ya hapa jiambie niko salama alafu hisi usalama, huku sauti inalia masikioni, huku unavuta picha kichwani ya rangi nyekundu.

ii.Tumbo(chini ya kitovu) rangi yake ni machungwa nota D(re), frequency 294 Hz, hisia ya hapa ni Ubunifu,jiambie mimi naweza kutengeneza furaha na hisia safi. Kwenye kichwa fikilia rangi ya machungwa huku sauti ikiendelea kulindima masikioni.

Fanya hivyo kwa chakra zingine

iii.Jua (tumbo la juu) manjano, nota E (mi), frequency 330 Hz, Hisia ya hapa ni Nguvu, jiambie mimi nina nguvu kamili ya kufanya maamuzi sahihi.

iv. Moyo (Kifua)kijani, nota F(fa) 349 Hz, hisia ya hapa ni upendo, jiambie ninatoa na ninapokea upendo bila masharti.

v.Koo(koo) Bluu G (so) 392 Hz , hisia ya hapa ni Ukweli,  jiambie mimi husema ukweli wangu kwa ujasiri na uwazi.

vi.Jicho la tatu (paji la uso) rangi ya Nili(Indigo) A (La) 440 au 432 Hz, hisia ya hapa ni Utambuzi , jiambie akili yangu ni wazi ninaona maono yangu kikamilifu.

vii.Taji(Juu ya kichwa) zambalau B (si/ti) 494 Hz , Hisia ya Muunganiko, jiambie mimi nimeungana na uungu.

Chakra ziko 7, sauti ya nota ilie angalau dakika 3 hadi tano kwahiyo ikiungana inakuwa audio yenye urefu wa dakika 21 au 35. Hata kama usipo fanikiwa kuvuta hisia ya Langi Fanya zoezi hili kwa wiki moja. Ukiona ni ngumu sana  kuvuta picha sikiliza sauti peke yake.

 

Hata kama unastress nzito kiasi gani sikiliza iyo audio kisha lala hakika utaanza kupata maono ya mazuri, na sio maono tu kiwango cha kuhisi na ufahamu wako utakuwa unaongezeka kila siku, uwezo wa kukumbuka ndoto utaongezeka. Hekima itaanza kuwa kubwa sana.

Kuna muda ukilala basi ndoto zinakuja mbaya , kama unaweza kupata mdarasini wakati unalala ile harufu yake iwe inakupiga , hata ukipitiwa na usingizi ndoto utazifurahia sana.

Hilo ni zoezi la kuthibiti frequency.

Ili uelewe jambo vizuri ni muhimu kulitafakari mara kwa mara. Kitendo cha kupitia masomo yangu mara moja moja hautapata nafasi ya kuunganisha nadhalia hizi ili ziweze kukusaidia katika maisha yako na ndio maana nakusihi uwe na kitabu changu cha mitetemo ya kiroho kwa maana kina kila kitu kwa mpangilio mzuri na inakuwa kama kumbukumbu na chanzo cha elimu kwa wanao kuzunguka.

Nimalize kwa kuku alika kununua kitabu changu cha MITETEMO YA KIROHO chenye gharama ya Tsh 25,000/= , kitabu ni nakala laini(eBook) unakipata kwenye Whatsapp yako baada ya kufanya malipo kwenye Namba 0682329852 ,

BASI UMEBARIKIWA KWA KUFANIKIWA KUPATA ELIMU HII KUBWA YA KIROHO.

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments